KUMI LA MWISHO KATIKA MWEZI WA RAMADHANI TUKUFU
wasifu
Mwenyezi Mngu Aliyetukuka Ametuwekea ibada tukufu katika kumi la mwisho la Ramadhani, zenye kuzidisha Imani na kufanya ibada zikamilike na neema kutimia. Ibada hizi ni Zaka za Fitri na Swala ya Idi. Ametuwekea Zaka za Fitri ili zimsafishe mwenye kufungana na maneneo machafu na matendo visivyo faa na ni chakula kwa masikini, na Ametuwekea Swala ya Idi ili kudhihirisha nguvu za Waislamu na umoja wao na vile wanavyo jikusanya pamoja.
Enyi Waislamu, Siku za mwezi mtukufu wa Ramadhani zinaendelea kuisha. Na hivi karibuni tutaanza kumi la mwisho. Je ndugu yangu Muislamu umejiuliza suala moja; Je nimefaidika kiasi gani na siku zilizopita? Kuwa mkweli na nafsi yako na ujifanyie hisabu ya vitendo vyako kabla hujafika siku ya kufanyiwa hisabu. Ndugu Muislamu, bado wakati upo, na fursa ya kufanya mambo ya kheri bado inaendelea.
Je umejiandaa kiasi gani na umejipangia mikakati gani katika kumi la mwisho? Kwa hakika ni siku muhimu katika umri wa mwanadamu, ndani yake kuna usiku mtukufu. Mwenye kuafikiwa usiku huo basi amepata kheri ya dunia na akhera. Na mwenye kukosa usiku huo basi amekosa kheri ya dunia na akhera. Ni khasara ilioje mtu kuishi duniani miaka mingi kisha aondoke duniani patupu bila ya kupata kheri ya dunia wala kheri ya akhera. Ndugu Muislamu tafakari na uzingatie, hujui kama utafika mwakani ili uweze kufunga Mwezi wa Ramadhani.
Watu wema walikuwa wakimuomba Allah mwaka mzima awaafikie kuweza kuzifikia siku hizi za kheri. Na wakifikiwa na siku hizi huwa na furaha nyingi, kwa kupata bahati ya kuishi mpaka kuweza kufunga Mwezi wa Ramadhani. Ndugu Muislamu Mtume Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) Ametufundisha mambo mengi na ibada nyingi ambazo Muislamu anaweza kuzifanya kwa ajili ya kujikurubisha kwa Allah (Subhaanahu wa Taala). Katika Ibada hizo ni kama ifuatavyo:-


Comments
Post a Comment