Swalah ya Janeza
Kumtayarisha Maiti
Inapendekezwa kuhudhuria pale penye mtu ambaye alama za kifo zimedhihiri kwake, na kumkumbusha kusema «Laa ilaaha illa-llah» kwa kauli yake Mtume ﷺ (Walakinini maiti zenu “Laa ilaaha illa- llaah”) [Imepokewa na Muslim.].
Akifa atafumbwa macho yake na afinikwe nguo na kufanywe haraka kumtayarisha kwa mazishi na kumswalia na kumzika.
Hukumu ya kumuosha maiti na kumtayarisha na kumzika
Kumuosha maiti, kumkafini, kumbeba, kumswalia, na kumzika ni katika faradhi inayotosheleza. Wakifanya baadhi ya waislamu inapomoka madhambi kwa waliobakia.
Hukumu ya kumuosha maiti
1. Yatakikana achaguliwe mtu mwaminifu wa kuosha maiti, pai awe mjuzi wa hukumu za kuosha.
2. Hutangulizwa kuosha yule mtu ambaye maiti mwenyewe alikuwa ameusia aoshwe na yeye. Kisha yule aliye karibu zaidi na maiti, iwapo ana ujuzi wa hukumu za kuosha. Akitokuwa hivyo, basi atatangulizwa mwenye ujuzi wa hilo.
3. Mwanamume huoshwa na wanaume, na mwanamke huoshwa na wanawake. Na kila mmoja miongoni mume na mke anafaa kumuosha mwenzake, kwa kauli ya Mtume ﷺ kumwambia›Aishah t: (Hakuna cha kukudhuru, lau wafa kabla yangu nikakuosha, nikakukafini na nikakuswalia kisha nikakuzika) [Imepokewa na Ibn Maajah.].
Pia inafaa kwa wanaume na wanawake kuwaosha watoto walio chini miaka saba. Na haifai kwa Muislamu - awe mwanamume au mwanamke- kumuosha kafiri, walakubeba jeneza yake wala kumkafini wala kumswalia, hata kama ni jama yake wa karibu kama vile baba.
4. Shahidi aliyekufa vitani haoshwi wala hakafiniwi wala haswaliwi, bali huzikwa na nguo zake.
5. Afikapo tisha- naye ni mwana aliyetoka kwenye tumbo la mamake kabla ya kutimia umbo lake, awe ni mwanamume au ni mwanamke- miezi minne, ataoshwa, akafiniwe na aswaliwe. Kwani yeye baada ya miezi minne huwa ashakuwa na umbo la binadamu kamili.
6. Maji ya kuoshea maiti ni sharti yawe ni maji yanayofaa kujitwahirishia na yawe ni ya halali, na aoshwe mahali pa sitara, na haifai kuhudhuria asiyekuwa na mafungamano yoyote na kumuosha maiti.
Namna ya kumuosha maiti
1. Maiti awekwe juu ya kitanda cha kuoshewa, kisha afinikwe uchi wake, kisha avuliwe nguo zake, afichwe na macho ya watu ndani ya chumba au mfano wake.
2. Inapendekezwa kwa muoshaji atatie kitambaa mkononi mwake wakati wa kuosha.
3. Muoshaji atakiinuwa kichwa cha maiti akaribie kumkalisha, kisha apitishe mkono wake kwenye tumbo lake na alikamue, kisha aisafishe tupu yake ya mbele na ya nyuma kwa kuosha najisi yoyote iliyopo.
4. Muoshaji atanuilia kuosha na atapiga bismillahi.
5. Muoshaji atamtawadhisha maiti kama udhu wa Swala, isipokuwa katika kusukutua na kupaliza puani, huwa inatosha kumpukusa kinywa na pua.
6. Atakiosha kichwa cha maiti na ndevu zake kwa maji ya mkunazi au sabuni au kinginecho.
7. Ataosha sehemu ya kulia kisha sehemu ya kushoto, kisha atakamilisha sehemu ya mwili iliyosalia.
8. Inapendekezwa atie kafuri katika osho la mwisho.
9. Atampangusa maiti.
10. Amuondolee maiti vitu vinavyotakikana kuviondoa kama kucha, nywele za kinena (nywele za sehemu ya siri) na makapwa.
11. Atazisuka mkili nywele za mwanamke aziweke nyuma yake
Atamuinuwa muoshaji ichwa cha maiti
Atatie muoshaji kitambaa mkononi mwake
Atawekwa maiti juu yakitanda cha kuoshewa
Muoshaji atabonyeza kwa mkono wake tumbo la maiti na kumkamua kwa upole
Muoshaji atamtawadhisha maiti kama udhu waswala
Atamuosha kichwa cha Maiti na ndevu zake kwa maji na mkunazi
Atamuosha upande wakulia kisha upande wakushoto
Atampanguswa maiti
Faida
- Lawajibu ni osho moja iwapo litatosha kumsafisha, na linalopendekezwa ni kumuosho mara matatu, hata kama ashasafishika.
- Ikitowezekana kumuosha maiti kwa kukosekana maji au ukiwa mwili umekatikakatika kwa moto au mfano wake, atatayamamishwa kwa mchanga.
- Inapendekezwa kwa mwenye kumuosha maiti aoge baada ya kumaliza kuosha.
Comments
Post a Comment