KUAMINI MITUME WA ALLWAH WALIO MTANGAZA .
KUAMINI MITUME WA ALLWAH WALIO MTANGAZA
Hakuumba Allwah Waja Wake Bure Tu Bila Sababu, Na Wala Hakuwaacha Bure, Ndipo Aliwatumia Mitume Wake Ili Wamtangaze Allwah, Na Utukufu Wake, Na Ukamilifu Wake, Na Kutangaza Sharia Zake, Na Allwah Ametuma Katika Kila Watu Mbora Wao ,Akatuma Mitume Mingi Sana Miongoni Mwao: Nuh Ibrahim,Musa,Issa, (A.S) Na Mwisho Akamtuma Mwisho Wa Manabii, Mbora Wa Viumbe Wote Muhamad (S.A.W) Na Akawapatia Kila Mmoja Miujiza Yake Yenye Kujulisha Ukweli Wao, Wakafikisha Amana, Na Wakatekeleza Jukumu La Utume, Na Wakawafahamisha Waja Kuhusu Mola Wao Na Muumba Wao, Basi Asie Amini Risala Yao Na Kutokubali Hajamuamini Allwah. Amesema Allah: {Mtume Ameamini Yaliyoteremshwa Kwake Kutoka Kwa Mola Wake, Na Waislamu, (Pia Wameamini Hayo): Wote Wamemwamini Mwenyezi Mungu, Na Malaika Wake Na Vitabu Vyake, Na Mitume Yake} (Al Baqarah 285)
Kwasababu Wao Ndio Walio Tufikishia Ujumbe WA Allwah Mtukufu Kwahiyo Tunawaamini Wote. Allah Amesema: {Hatutafautishi Baina Ya Yoyote Katika Mitume Yake (Wote Tunawaamini)} (Al Baqarah 285)
Allwah Mtukufu Ametuma Hawa Mitume Pamoja Na Vitabu Ili Viwe Nuru Kwa Wanadamu, Akatuma Pamoja Na Nabii Ibrahim Sahifa Na Pamoja Na Nabii Daudi Zabuur Na Pamoja Na Nabii Na Musa Taurat, Na Pamoja Na Nabii Issa Injil Na Pamoja Na Mtume Muhamad (S.A.W) Quran Kitabu Kilicho Na Miujiza: {Hiki Ni Kitabu Ambacho Aya Zake Zimetengenezwa Vizuri, Kisha Zikapambanuliwa (Vyema) Kutoka Kwa (Mwenyezi Mungu) Mwenye Hikima Na Mwenye Ujuzi Wa Kila Kitu.} (HUD 1)
Amekifanya Allah Kuwa Ni Uongofu Na Nuru Na Baraka Na Dalili. Asema Allah Mtukufu: {Na Hii Qurani Ni Kitabu Tulichokiteremsha (Kwenu), Kilicho Na Baraka Nyingi. Basi Kifuateni Na Muwe Wacha Mungu Ili Mrehemewe} (Alan-Am 155)
Na Akasema Tena: {Enyi Watu! Imekufikieni Dalili Kutoka Kwaa Mola Wenu, Na Tumekuteremshieni Nuru Iliyo Dhahiri} (An Nisaa 174)
Allwah Amejalia Kuamini Mtume Muhamad (S.A.W.) Na Kuamini Ujumbe Wake Kuwa Pamoja Na Kumuamini Yeye Pekee, Katika Kalma Ya Shahada Ambayo Ni Kushuhudia Kuwa Hakuna Apaswaye Kuabudiwa Kwa Haki Illa Allah, Na Kushuhudia Kuwa Muhamad (S.A.W) Ni Mtume Wake, Amemtuma Allwah Mtukufu Kuwa Rehema Ya Walimwengu, Akawatoa Kutoka Giza Paka Kwenye Nuru, Na Kutoka Kwa Ujahili Paka Kwa Elimu Na Kutoka Kwa Upotevu Paka Kwenye Uongofu, Akafikisha Amana Na Akawanasihi Watu Na Alikuwa Na Pupa Juu Ya Umma Wake , Amesema Allah Mtukufu: { Amekufikieni Mtume Aliye Jinsi Moja Na Nyinyi, Yanamuhuzunisha Yanayokutaabisheni, Anakuhangaikieni. (Na) Kwa Walioamini Ni Mpole Na Mwenye Huruma} (At Tawba 128)
Allah Akampa Mtume Wake Miongoni Mwa Haki Anazostahiki, Yeye Ni Mbora Wa Viumbe Vyote Na Bwana Wao, Asema Mtume (S.A.W) &" Mimi Ni Bwana Wa Watoto Wa Adam Wala Sikujisifu.&" (Imepokewa Na Ibn Maja)
Comments
Post a Comment