Tamasha za idd ya fitri
Tamasha za idd
Idi za Waislamu ni mbili: Idi ya Fitri baada ya mwezi wa Ramadhani na Idi ya Adh›ha baada ya siku ya Arafa. Na Mwenyezi Mungu Ametupa Idi hizo ziwe ni badala ya Idi za kijahilia na kila idi yenye kuzuliwa. Anas bin Malik t amepokewa akisema: «Watu wa Jahilia (kabla ya Uislamu) walikuwa na siku mbili kila mwaka, wakisherehekea idi hizo. Mtume ﷺ alipokuja Madina alisema: (Mlikuwa na siku mbili mkizisherehekea, na Mwenyezi Mungu Amewabadilishia idi bora kuliko hizo: Idi ya Fitri na Idi ya Adh’ha) [Imepokewa na Nisaa.].👇👇
https://www.al-feqh.com/sw/swala-ya-idi-mbili
Comments
Post a Comment